Machapisho

KWEPA FITINA KWA UPENDO

Picha
                       KWEPA FITINA KWA UPENDO Bwana asifiwe karibu tujifunze tena asubuhi ya Leo.. Biblia Inaweka wazi jinsi ya kukimbia fitia au kuikwepa miongoni mwa watu... Haebu soma hapa 👇 Mithali 10:12 [12]Kuchukiana huondokesha fitina;  Bali kupendana husitiri makosa yote.  Kumbe kama chuki Inasababisha kuwe na FITINA basi njia sahihi Kwa hapa ni Kutokuwa na chuki kati au baina ya watu... Kukiwa na chuki miongoni mwa rafiki, kikundi au watu basi haya yaweza kutokea... 👉Kila mtu atatamani kumchafua mwenzake ili afunge kibali chake  👉Kila mtu hatamuona mwingine kama msaada bali adui  👉Kila mtu atamtazama mwenzake kama chanzo cha huzuni yake 👉Moyo wa mtu na mtu wanaochukiana huwa hauwezi kukaa pamoja 👉Hakuna mtu atakuwa tayari kumsaidia mwenzake   👉Watu hawa wanaweza kushindwa kukosa fursa kwasababu mara zote fursa inayotengenezwa na Mungu huja kwa mtu kupitia watu Na mbaza nyingine ni kwamb...

UVUMILIVU UTAKUVUSHA TAABUNI

Picha
                 UVUMILIVU UTAKUVUSHA TAABUNI Bwana asifiwe karibu tujifunze tena hapa UVUMILIVU ni tunda la Roho ambalo ni lazima kila mtu wa Mungu alijue na awe nalo kwasababu linakufanya nafsi yako iwe na utulivu kwa Bwana hata kama unapitia taabu... Tambua kwamba taabu ni sehemu ya maisha ya kila mtu, yaani 👉Kuna wakati wa kukosa na wakati wa kupata 👉Pia Kuna wakati wa kuwa chini, 👉wakati wa kudharauliwa, 👉 wakati wa kutenga, 👉wakati wa kukosa kazi n. K Yaani hayo hayakwepeki... Lakini cha msingi ni kujua kwamba hayo yote yana muda fulani wala si ya kudumu.. Taabu zina uwezo wa kumfanya mtu kurudi 👉Wengine hurudi nyuma kwenye wokovu kwasababu wametafuta kazi kwa muda bila kupata wakaona kana kwamba Mungu wao hawaoni 👉Wengine huacha wokovu kwasababu tu ya magonjwa 👉Wengine hurudi nyuma kwa kukosa Mume au mke kwa muda mrefu 👉Wengine hurudi nyuma kwasababu ya njaa tu... Lakini mambo hayo hayapaswi kabisa kututenga na ...

MAFANIKIO SIYO AJALI NI MATOKEO

Picha
    MAFANIKIO  SIYO AJALI NI MATOKEO Bwana asifiwe karibu tujifunze tena hapa asubuhi njema... Tunaishi kwenye maisha ambayo ya a watu wawili katika viwango vya kimaisha yaani maskini na tajiri na mara zote kila mtu hutamani kuwa tajiri kwenye maisha yake ili aweze kujimudu na kuendesha maisha yake vizuri... Lakini je unajua kuwa utajiri na umaskini siyo ajali??? Hali hizi mbili ni matokeo ya utendanji kazi, kufikiri na imani ya mtu mwenyewe.. Umaskini huanzia katika akili, kisha imani na mwisho kuongoza utendaji kazi wa mtu na hata umaskini kujidhihirisha kwa mtu... Katika kutenda kazi hapa Kuna uvivu na uhodari, Biblia inasema hivi 👇  Mithali 10:4 Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha.  [4] Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini;  Ukiwa unafanya kazi kivivu na Huku unatarajia ustawi basi tambua unaidanganya nafsi yako  Mafanikio ya kiuchumi hayahitaji maombi bila kufanya KAZI kwa bidii, ukikaa ndani, ukafunga na kuomba kwa bidii haina ma...

ATAKULETA HUKUMUNI

Picha
                                                               ATAKULETA HUKUMUNI Bwana asifiwe wana wa Mungu, njoo tujifunze tena Ni dhahiri katika maisha haya watu wa rika zote hususani vijana na watu wazima, wana mambo yao na shughuli zao ambazo hupenda kuzifanya za kuwafurahisha mioyo yao hapa duniani Hebu tusome hapa👇 Mhubiri 11:9-10 [10]Kwa hiyo ondoa majonzi moyoni mwako, nawe uuondoe ubaya mwilini mwako; kwa maana ujana ni ubatili, na utu uzima pia.  [9]Wewe kijana, uufurahie ujana wako, na moyo wako ukuchangamshe siku za ujana wako, ukaziendee njia za moyo wako, na katika maono ya macho yako, lakini ujue wewe ya kwamba kwa ajili ya hayo yote Mungu atakuleta hukumuni.  Hapo biblia inazungumza na watu wawili kwasababu kwa asilimia kubwa watu hawa ndio Taifa la sasa yaani vijana na watu wazima.. Sasa kijana ni mt...

SHERIA YA MUNGU NI UZIMA SIYO UDIKTETA

SHERIA YA MUNGU NI UZIMA SIYO UDIKTETA Bwana asifiwe karibu tujifunze tena katika asubuhi ya Leo jumapili... Kuna watu wengi naamini huwa wanajiuliza au walishawahi kujiuliza maswali haya hapa👇👇 👉Kwanini Mungu ameweka sheria nyingi za kumuongoza mtu??  👉Mbona kama mtu hana uhuru wake mwenyewe??  👉Mbona Mungu anawaongoza watu kama dikteta kwa amri fulani fulani nyingi??  👉Mbona mambo ya Mungu yana taratibu nyingi sana za kuzitii ??? 👉 Mbona biblia imejaa makatazo mengi sana ya Mungu kwa mwanadamu??? Sasa nilazima ujue kwamba yote aliyoyasema Mungu kwa watu wake... Si tu kwasababu anataka umuheshimu kwa kuyatii lakini mambo hayo ni ufunguo wa mambo fulani katika roho   Kwa mfano Mungu aliposema USIZINI si kwamba amekutawal kidikteta  lakini anajua ukifanya uzinzi si tu kwamba unamkosea yeye bali Kuna madhara makubwa sana utayapata ambayo ni matokeo ya zinaa hata kama atakusamehe ukitubu... Ukitubu, Mungu anakusamehe dhambi lakini madhara ya dhambi hiyo utab...

KAMA MUNGU ANAJIBU MAWAZO KWANINI TUNAOMBA??

Picha
KAMA MUNGU ANAJIBU MAWAZO KWANINI TUNAOMBA ?? Na: Minister Mathayo Sudai Bwana asifiwe karibu tujifunze tena hapa... Katika somo la nyuma tulijifunza kwamba Mungu ANAJIBU MAWAZO YAKO SIYO MANENO YAKO... Kama hujalipitia somo hili ni vizuri ukalipitia ili ukija Kuendelea uwe unaelewa vizuri... Bofya link hii hapa kwa somo hilo kabla hujaendelea na hili👇👇 https://elimuyabiblia.blogspot.com/2025/03/mungu-anajibu-mawazo-yako-siyo-maneno.html Kama umeshaelewa njoo tuendelee... Tuliishia kwenye kujiuliza 👉Kama ni hivyo kwamba Mungu anajibu mawazo Kuna haja gani ya kuomba??? 👉Je nikiwa nawaza tu pekeyake si inatosha mimi kupata majibu?? Lakini tukasema Jibu ni kwamba Japo kuwa Mungu ameyajibu mawazo yako lakini majibu yako hutayapata mkononi mwako mpaka utakapoomba(kutamka uliyokuwa unawaza) 🤔🤔 SASA Ili kuelewa hapa ni lazima tukubaliane na Biblia kwamba Mungu anapohitaji kumuhudumia mwanadamu huwa hafanyi yeye bali watumishi wake ndiyo huwa wanafanya kazi hiyo na watumish...

MUNGU ANAJIBU MAWAZO YAKO SIYO MANENO YAKO...

Picha
MUNGU ANAJIBU MAWAZO YAKO SIYO MANENO YAKO... Min Mathayo Sudai Bwana asifiwe wana wa Mungu... Njoo tujifunze kuhusu jinsi Mungu anavyoyatazama mawazo yako, na ukilijua hili hautadharau mawazo yako tena.... Kimsingi Mungu na Shetani wanapenda au hutenda kazi kupitia ulimwengu wa mawazo ya mtu yaani jinsi unavyowaza... (The realm of thoughts) Isaya 65:24 [ 24]Na itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia. Unaona kujibiwa kunaanza hata kabla ya mtu kutamka kile anachokihitaji... Kwasababu kile ambacho unakitamka ni matokeo ya vile unavyowaza, kabla hujaanza kuomba ni lazima utawaza kile kitu ambacho utakiomba... Kwa mfano.                                                                                             ...

KAMA BWANA ASINGALIKUWA MSAADA WANGU....

Picha
KAMA BWANA ASINGALIKUWA MSAADA WANGU.... Min. Mathayo Sudai Bwana asifiwe wana wa Mungu  Karibu tujifunze neno la BWANA Tuanze hivi👇 Zaburi 94:17 [ 17]Kama BWANA asingalikuwa msaada wangu, Nafsi yangu kwa upesi ingalikaa penye kimya. Ulimwengu huu umejawa na mambo mengi sana ya ajabu ambayo yanalenga kuangamiza nafsi za watu, na kuwatoa watu nje ya makusudi ya Mungu... Kimsingi Mungu wetu ni mwaminifu kwasababu huilinda nafsi ya kila mtu mwenye dhambi na hata aliyeokoka na ndiyo maana watu wote hao wapo duniani.... Ni kweli kabisa kwamba kama Mungu asingekuwa anamlinda mtu basi wanadamu wangeshawekwa palipo na kimya (mautini)... Hapo Daudi anakiri kwamba kuishi kwake yeye ni Mungu tu na kama isingekuwa hivyo basi yeye asingekuwepo yaani angeshakufa muda mrefu.. Si Daudi tu, unaweza kujiangalia wewe mwenyewe hapo ukaelewa kwasababu 👉Kama si mkono wa Mungu uliokuvusha kwenye ile kesi basi muda huu huenda ungekuwa jera 👉Kama si Mungu kuwa upande wako pengine ungeuawa k...

KWANINI ULIMWENGU HAUKUMKUBALI YESU ANGALI YEYE NDIYE ALIYEUUMBA???

Picha
KWANINI ULIMWENGU HAUKUMKUBALI YESU ANGALI YEYE NDIYE ALIYEUUMBA??? Bwana asifiwe, karibu tujifunze... Biblia inasema hivi 👇 Yohana 1:10-11 [ 10]Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua. [11]Alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea. Tunaposoma biblia Kuna kitu cha msingi tunakiona hapo kwamba Yesu ndiye aliyehusika kuumba ulimwengu lakini inaonekana alipokuja ulimwenguni tena ulimwengu aliouumba mwenyewe na siku zote yupo humo lakini ulimwengu haukumtambua na hata wale ambao walikuwa wake walimkataa yaani hawakumpokea.. Je ni kwanini??? Ni jambo la ajabu sana kama umemzaa mtoto halafu baadae anakuwa hakujui tena na hata ukimfuata anakukataa yaani hakupokei bila shaka ni lazima Kuna kitu ambacho kimempata mtoto huyo maana si kawaida.... NI HIVI👇 Adamu alipoumbwa na Mungu (kristo Yesu ), ulimwengu ulikuwa chini yake na kila kitu kilikuwa sawa maana nuru ya Mungu ilikuwepo lakini baada ya shetani kumdanganya Adamu na kufan...

TAFUTA KUKUA, USIRIDHISHWE NA SHETANI

Picha
TAFUTA KUKUA, USIRIDHISHWE NA SHETANI Na:Minister Sudai Bwana Yesu asifiwe sana watu wa Mungu, karibu tujifunze kitu cha msingi kuhusu kukua kiroho... Soma hapa👇 Wakorintho 13:11 [11]Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto. Hapa Paulo anazungumza jinsi ambavyo unapaswa kuwa na utofauti kwa jinsi ulivyokuwa mtoto na ulivyo Leo... Jambo hili ni la kulitazama zaidi kwa mambo ya rohoni kwasababu kabla hujawa mtu Mzima kiroho ni lazima uwe mtoto na si ajabu biblia inalithibitisha hilo.....👇 Waebrania 5:13-14 [13]Kwa maana kila mtu atumiaye maziwa hajui sana neno la haki, kwa kuwa ni mtoto mchanga. [14]Lakini chakula kigumu ni cha watu wazima, ambao akili zao, kwa kutumiwa, zimezoezwa kupambanua mema na mabaya. Unaona hapo...?? Mtu mzima si mtu aliyeokoka muda mrefu au Ana umri Mkubwa bali kunahusisha sana jinsi anavyoenenda kwa mambo ya ...

NA WEWE HUIPENDI HEKIMA ??

Picha
  NA WEWE HUIPENDI HEKIMA ?? Bwana Yesu asifiwe  njoo tujifunze kitu kizuri Leo kwa msaada wa Mungu  NI HIVI 👉Hekima huwa ni jibu kwa maswali mengi Sana... 👉Hekima inaweza kumlinda mtu mwenye nayo... kama vile fedha ilivyo na nguvu ndivyo Hekima ilivyo na nguvu pia kwa Mwenye Hekima.. Muhubiri 7:12 Kwa maana hekima ni ulinzi, kama vile fedha ilivyo ulinzi; na ubora wa maarifa ni ya kwamba hekima humhifadhi yeye aliye nayo. 👉Hekima inaweza KUMPA mtu njia ya Nini afanye pale anapokutana Na jambo linalotaka uamuzi  👉Hekima inaweza kumfanya mtu akawa salama kaka ataisikiliza  👉Hekima inaweza KUMPA mtu Mali nyingi katika Dunia hii... 👉Hekima inaweza kumfanya mtu akafatwa na watu ili awafundishe hekima 👉Hekima inaweza kufanya Mali za wengine zikakuhudumia .... watu kutoka pande nyingi watakuja na mali zao kwako na weweutajivunia Utajiri wa watu wa mataifa .... Soma habari za suleimani... malkia wa sheba alikuja na wengine wengi pamoja na mali zao ili kuiona na ...

SI KILA SILAHA INATUMIKA SEHEMU ZOTE...

Picha
SI KILA SILAHA INATUMIKA SEHEMU ZOTE... Bwana asifiwe Wana wa Mungu.. Leo naomba nikushirikishe habari ya Vita ya kiroho na hapa nazungumzia kuhusu siraha za vita hiyo... moja ya vitu ambavyo tunatakiwa kuvijua na kujua jinsi ya kuvitumia ni silaha za kiroho .... maana ukishindwa basi unaweza kujikuta unapigwa kwasababu huzijui au hujui jinsi ya kuiitumia... kimsingi Vita ya kiroho ni jambo ambalo kanisa limelipuuzia Sana kiasi kwamba wakristo wengi hawaelewi chochote kuhusu Vita ya kiroho na wanabaki kushangaa tu pale wanapionanmambo hayaendi au kuharibika... hebu tuone silaha za milele na sehemu ya kuzitumia... hapa nazungumza kuhusu  👉jina la Yesu  👉Damu ya Yesu na  👉Neno la Mungu .... Kuna silaha nyingi za kumlinda mtu na kushambulia pia kulingana na Waefeso 6.. 1. Unapohitaji  👉kukemea pepo basi ni kwa jina la Yesu  👉kuombea wagonjwa ni kwa jina la Yesu  👉kunena kwa Lugha mpya ni kwa jina la Yesu  👉Kukanyaga nyoka na ng'e ni kwa jina la Yes...

USIMSAHAU MTOTO.

Picha
                     USIMSAHAU MTOTO. Bwana asifiwe watu wa Mungu... Leo naomba tutazame juu ya watoto na kile tunapaswa kuwafanyia ili wawe Salama.... Mithali 22:6   Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee. MTOTO ni mtu ambaye haijafika katika hatua ya kujisimamia, yaani bado anahitaji kufanyiwa kila kitu ili awe Salama... 👉MTOTO anahitaji kununuliwa nguo 👉kufuliwa.. 👉kuogeshwa  👉na kila kitu ambacho Mwanadamu anakihitaji isipokuwa yeye anatafanyiwa hayo yote.  mtoto anahitaji hayo katika Masha yake, na hayo yote anatakiwa kupewa au kufanyiwa na mtu mzima asiye  mtoto kama yeye.... lakini Kuna kitu Cha msingi Sana kwa watoto kinaitwa MALEZI.. MALEZI ndilo japo linalotengeneza njia ambayo mtoto anaifuata... kimsingi mtoto Hana uwezo wa kuchagua njia ya kupita, lakini mtu mzima lazima awepo ili kumwonyesha njia na kumsimamia mpaka pale atakapokuwa amekuwa na uwezo wa kujisim...

SI KWAAJILI YA NDOA BALI NI ASILI YAKO MWANAMKE

Picha
SI KWAAJILI YA NDOA BALI NI ASILI YAKO MWANAMKE  Bwana asifiwe mabinti wa Mungu...  Leo naomba nikukumbushe juu ya sifa ambazo mwanamke anafaa awe nazo ili awe mwanamke mzuri ..... sifa hizi si kwasababu unahitaji kuolewa, au unataka kudumu kwenye ndoa... sifa ambazo Unatakiwa kuwa nazo pia si zawadi au karama ambazo zinatoka kwa Mungu.... Bali ni nilitihada zako Binafsi na huku ukilifuata Neno la Mungu.... Neno la Mungu ndio msingi sahihi wa tabia au sifa ambazo Unatakiwa kuwa nazo... ziko nyingi Sana Lakini Leo tuangalie kadhaa... 1 Petro 3:3-6 " Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu. Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao. Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mem...

MWANAMKE, USIKAE KINYONGE WEWE SI DHAIFU

Picha
MWANAMKE, USIKAE KINYONGE WEWE SI DHAIFU Na: Minister Mathayo Sudai  Bwana asifiwe mabinti Safi wa Yesu... Kuna mambo mengi Sana huwa yanafanyika katika Dunia hii na mwanamke huwekwa katika nafasi ya mwisho jambo linalopelekea kusomeka kama mtu ambaye ni dhaifu ... lakini vile mambo yanavyoenenda mara nyingi katika Dunia hii iliyoaanguka huwa ni kinyume kabisa na vile ambavyo Mungu anatazama na kutamani... KIMSINGI 👉Mwanamke ni imara kuliko Mwanaume 👉Mwanamke ana msimamo na si rahisi kukata tamaa zaidi ya Mwanaume 👉Wanawake Wana nguvu Sana kuliko na jinsi wanavyotazamwa... 👉Mwanamke Akiwepo nyumbani basi hata mgeni akifika anajua kwamba nyumba ina mwanamke.... na jambo la msingi ni kwamba katika Dunia hakuna Mwanaume hata mmoja anayeweza kumjua kiundani mwanamke... hayupo .. kwasababu mwanamke ni fumbo.... (Mwanzo 2:21) 👉mwanamke ni lango la baraka fulani kutoka kwa Mungu ambazo Mwanaume hataweza kupata mpaka atakapokuwa amemuoa  mwanamke huyo....  Mithali 18:22...

IJUE MITHALI 18:24

Picha
IJUE MITHALI 18:24 Bwana Yesu asifiwe... Leo tuangalie mstari huu wa Mithali 18:24 tujue Mungu anasema Nini kupitia eneo hili kwenye maisha yetu.... Soma hapa.... Mithali 18:24   Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu. hapo Kuna mambo mawili ya msingi sana ambayo inatakiwa tuyajue... 1. kujifanyia rafiki wengi ...     katika jamii au maisha Kuna kitendo cha mtu kupata au kuwa na mtu mwingine wa karibu yaani rafiki... katika hili inatakiwa kuelewa kwamba kila mtu ambaye utamruhusu aingie kwenye maisha yako kama rafiki basi jua ana mchango fulani kwenye maisha yako ..(ana influence fulani)... na sehemu kubwa ya shida au matatizo watu wengi wanapitia ni kwasababu ya rafiki zao au aina ya watu walioambatana nao yaani 75% ya shida watu hupata kutokana na watu waliowaweka Katibu Yao.....  👉wengine huingizwa kwenye makundi mabaya na rafiki zao 👉wengine hufundishwa njia ya kuishi na rafiki zao.. 👉we...

IJUE MAANA SAHIHI YA KUPENDA

Picha
     IJUE MAANA SAHIHI YA KUPENDA ... Bwana asifiwe... njoo tujifunze kitu kuhusu upendo hapa na jinsi ya kujua kama una upendo.... UPENDO ni jambo la kiroho, kimwili, kihisia na kimatendo lililopo kati ya watu..   MATENDO huambatana na Hali na MATENDO mbalimbali kama vile 👉kuhudumiana, 👉 kuthaminiana,  👉kutii, 👉kujali na  👉kuwa tayari kuwa pamoja katika mapito mbalimbali... UPENDO haupo mdomoni tu, yaani isiishie kusema una upendo Bali inatakiwa ufikie hatua ya kuuonyesha upendo... kwamfano... tunapokuwa tunasema tunampenda Mungu, haitakiwi kutamka tu Bali upendo wa Mungu ni kuzishika amri zake yaani kufanya sawasawa na maagizo ya Mungu.... ( MATENDO lazima yahusike ) Yohana 14:21 [21]Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake. unaona hapo kumbe kumpenda Mungu siyo lazima useme au umwambie Mungu, Bali kitendo Cha kushika Sheria zake na kutenda saw...