ATAKULETA HUKUMUNI
ATAKULETA HUKUMUNI
Bwana asifiwe wana wa Mungu, njoo tujifunze tena
Ni dhahiri katika maisha haya watu wa rika zote hususani vijana na watu wazima, wana mambo yao na shughuli zao ambazo hupenda kuzifanya za kuwafurahisha mioyo yao hapa duniani
Hebu tusome hapa👇
Hapo biblia inazungumza na watu wawili kwasababu kwa asilimia kubwa watu hawa ndio Taifa la sasa yaani vijana na watu wazima..
Sasa kijana ni mtu anaishi katika ulimwengu wa ujana, n mtu mzima pia katika ulimwengu wa utu uzima ambapo sehemu zote Kuna mambo yao na viburudisho vyao ambavyo hufarahisha mioyo yao..
Lakini Mungu Kuna kitu cha kutisha amekisema hapo... Amesema hivi UJANA NA UTU UZIMA NI UBATILI...
Kama ujana na utu uzima ni ulimwengu au hatua ambazo watu hhuzipitia, na hatua hizo au maeneo hayo ni UBATILI, hii inamaanisha kuwa mtu anapofika katika hatua hizo moyo wake unajazwa mambo ya eneo hilo yaani mambo ya ujana au utu uzima ambapo mambo hayo ni UBATILI.. Kumbe katika hatua hiyo mtu hatakiwi kufuata mambo ya moyo wake bali afuate mambo na maneno ya Bwana... Kwasababu kwa hayo na hizi hatua Mungu huwahukumu watu...
Na ndiyo maana akasema hukatazwi kujifurahisha, au kutufurahisha moyo uwapo kwenye ujana au utu uzima lakini ujue na ukumbuke na uwe na hakika Moyoni mwako kwamba kwa hayo yote Mungu atakuhukumu.. Yaani Mungu atahukumu kwa kutazama kile utendacho...
Kumbe kila unachokiita starehe na burudani za ujanani ni UBATILI hivyo kuwa makini, acha kufuata moyo bali fuata neno la Mungu
Biblia imeongea kwa njia ya tofauti sana kwenye eneo hili... Anawaruhusu watu waziendee njia za mioyo yao na kujifurahisha lakini katika yote wajue Bwana atawaleta HUKUMUNI katika hayo...
Na ndiyo maana Mungu akasema jinsi ambavyo mtu anatakiwa kuifuata njia iliyonyooka..
Je wewe unaifuta njia gani?? Ni njia ya moyo wako au njia ya Mungu?? Basi ifuate njia ya Mungu ili uwe salama kwenye maisha ya sasa na ya milele..
Mungu akubariki sana
Maoni
Chapisha Maoni